Aliyekuwa Mwakilishi wa Kiembesamaki,
Mansour Yussuf Himid
|
Pinda alilijibu kwa kifupi huku akimrushia kijembe
mbunge huyo kwa kusema kwamba si jambo la ajabu mwakilishi huyo kufukuzwa mbona
chama cha CUF kilimtimua mbunge wao.
“Si ajabu yaani kwa CCM tu, mbona nanyi
chama chenu kilifanya hivyo ingawa mbunge wenu bado ni mbunge?,” alihoji Pinda
kwa kifupi.
Agosti 26, mwaka huu Halmashauri Kuu ya Chama Cha Mapinduzi (NEC)
ilitangaza kuridhia kuvuliwa uanachama kwa Mansour kama ilivyopendekezwa na
Halmashauri Kuu ya chama hicho Mkoa wa Mjini Magharibi Zanzibar.
Hatua hiyo,
ilitokana na mjumbe huyo kukabiliwa na tuhuma akidaiwa kushindwa kusimamia
malengo ya CCM na kutekeleza masharti ya uanachama. Mengine kushindwa
kutekeleza wajibu wa mwanachama na kukiuka maadili ya CCM na Ilani ya CCM ya
mwaka 2010-2015.
Agosti 18, mwaka huu Kamati ya maalumu ya Halmashauri Kuu ya
CCM Zanzibar, ilipitisha mapendekezo ya kumvua uanachama mwakilishi huyo na
waziri wa zamani wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar.
No comments:
Post a Comment