Wasiliana nasi : chademadiaspora@gmail.com -Fair and Balanced Platform- Twitter @ChademaDiaspora

Wasiliana nasi : chademadiaspora@gmail.com -Fair and Balanced Platform- Twitter @ChademaDiaspora
----------------------WE THANK AND APPRECIATE YOU FOR VISITING CHADEMA DIASPORA BLOG. AGAIN, THANK YOU!-----------------------

Wednesday, March 20, 2013

LWAKATARE ATUPWA RUMANDE HADI APRIL 3 BAADA YA KUFUNGULIWA MASHITAKA UPYA


MAHAKAMA ya Hakimu Mkazi Kisutu Dar es Salaam imewafutia kesi ya makosa ya ugaidi  Mkurugenzi wa Ulinzi na Usalama wa Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Wilfred Lwakatare  na Ludovick Joseph baada ya Mkurugenzi wa Mashitaka( DPP), Dk Eliezer Feleshi kuwasilisha hati ya kuwafutia kesi hiyo washitakiwa kwa sababu hana haja ya kuendelea nayo.

Sambamba na hilo, DPP ilimfungulia kesi ya makosa ya ugaidi  upya Lwakatare na Ludovick ambapo kesi hiyo mpya namba  Na.6/2013 ambapo imepangiwa kwa hakimu mpya Aloyce Katemana. 

Katika kesi ya ugaidi Na.37/2013 iliyofunguliwa na Jamhuri dhidi ya Lwakatare na wenzake Machi 18 mwaka huu, ambayo ilifutwa saa tatu asubuhi na ambayo ilikuwa imekuja kwa ajili ya Hakimu Mkazi, Emilius Mchauru kuitolea uamuzi wa ama wa kuwapatia dhamana washitakiwa au la, hakimu Mchauru alijikuta akishindwa kutoa uamuzi wake kwa sababu  mawakili viongozi wa serikali Ponsian Lukosi, Prudence Rweyongeza na Peter Mahugo waliwasilisha  hati hiyo ya DPP chini ya kifungu cha 91(1) cha Sheria ya Mwenendo wa Makosa ya Jinai ya mwaka 2002, ambapo kifungu hicho kina mpa mamlaka DPP, kuifuta kesi yoyote ya jinai muda wowote kabla ya haijatolewa hukumu na uamuzi huo wa DPP haujahojiwa 

Source: Jackson A. (March 2013). Lwakatare atupwa Rumande hadi Apri 3, baada ya kufunguliwa mashtaka mapya. Retrieved from Audiface Jackson blog

No comments: