Wasiliana nasi : chademadiaspora@gmail.com -Fair and Balanced Platform- Twitter @ChademaDiaspora

Wasiliana nasi : chademadiaspora@gmail.com -Fair and Balanced Platform- Twitter @ChademaDiaspora
----------------------WE THANK AND APPRECIATE YOU FOR VISITING CHADEMA DIASPORA BLOG. AGAIN, THANK YOU!-----------------------

Saturday, May 18, 2013

CHADEMA yatisha Mbeya: Ni uchaguzi wa udiwani kata ya Iyela (airport)



Chama cha Chadema kimezindua kampeni zake leo za uchaguzi wa udiwani kata ya iyela kata hiyo imekuwa wazi bila diwani kwa muda wa miezi 5 sasa baada ya aliyekuwa diwani mzee Mkwenzulu kufariki dunia mwanzoni mwaka huu. CHADEMA mgombea wao ni Ndugu Charles Nkela na CCM mgombea wao ni mzee mmoja wa kihindi mwenye asili ya Pakstan maarufu kama Chan Van Cheng ambaye naye atazindua kampeni zake zake kesho jumamosi. CHADEMA walizindua kampeni kwa kuanza na maandamano makubwa kabisa yaliyoshirikisha watu zaidi 2000 hivi yalianzia eneo la Air port na kuishia uwanja wa soko la maendeleo katani hapo. Akizindua kampeni kiongozi mmoja wa CHADEMA Ndg Mwampiki ambaye ni katibu mwenezi wa CHADEMA wilaya Mbeya mjini alisema kata hiyo ni tajiri kuliko zote jijini mbeya lakini kutokana na usimamizi mbovu wa viongozi wa CCM watu wake wanaishi kimasikini kupita kawaida. 

Kata hiyo ndipo lilipo soko la sido la jijini Mbeya ina vyuo vikuu 2 kikiwemo Chuo cha Teku na tia pia ina mabenki 5 na ndipo ulipo uwanja wa ndege wa jijini Mbeya (sio songwe). Na barabara zake ni mbovu kuliko wakati kata ambaye yeye Mh. Mwampiki ni diwani (mwakibete) haina vyote hivyo lakini ameisimamia vizuri kiasi kufika mbali kwa kujenga shule ya Secondary yenye majengo 9 kwa kuwachangisha wananchi wake sh.3000/=@ na chenji ikabaki wakati kata hiyo ya Iyela diwani aliyepita alishindwa licha ya kuchangishi sh 10000/=@. Katika jiji la Mbeya michango ya ujenzi wa shule za secondary ni sh 10000/= @kwa kata zenye madiwani wa CCM na sh 3000/=@ kwa kata zenye madiwani wa CHADEMA ajabu ni kuwa kata za CHADEMA zinakamilisha ujenzi haraka na chenji inabaki na za CCM licha ya kuchangisha sh 10000/=@ zimeshindwa kukamilisha ujenzi huo na kukumbwa na kashifa mbalimbali ikiwemo wizi wa vifaa vya ujenzi wa shule mfano ni kata ya Igawilo ambayo Mh.diwani wa kata hiyo ambaye pia ni naibu meya wa jiji la Mbeya Ndg Chifoda Fungo alifikia kuiba hadi bati za shule ya kata yake ya Mponja. 

Hata hivyo alifanya yote hayo na analindwa na mkuu wa wilaya ya mbeya mjini Ndg Nolman Sigala inasemekana ni ndugu yake na wamesoma wote elimu ya secondary huko bulongwa Makete. Wanambeya kuweni makini chagueni mzalendo wa nchi hii na si wapenda ufisadi mkikosea itawagharimu.

No comments: